SIMBA : HUYU PEKEE NDIYE ANAWEZA KUMFANYIA TOHARA CHUI..

 SIMBA:HUYU PEKEE NDIYE ANAWEZA KUMFANYIA TOHARA CHUI.
Wakati fulani mwaka 2003..ilikuwa usiku wa jumapili fulani hivi,niliamshwa na kelele za baba yangu mzazi mzee Mayeka akipiga kelele na yowe lisilo la kawaida..ule “mzuka” wake na yale makelele yalituzindua usingizini mimi na kaka yangu ..katika akili yetu ya kitoto tuliamka na kabla ya kuhoji kilichotokea tiyari alikuwa akitamka maneno fulani kwa sauti ya juu akisema “jamani simba imeshinda..simba imeshinda misri..” sasa nikaanza kupata picha..asubuhi ya siku ile alikuwa ametusimamia kufanya zoezi la kuchimbia mlingotiwenye bendera yenye mistari ya rangi nyekundu na nyeupe..ambayo alikuwa ametoka kuinunua siku chache zilizopita..baada ya wiki chache zilizofuata alianza kutuchukua kwenye baiskeli yake na kwenda kijiji cha pili  kuiangalia ile timu yake ilomfanya ajitoe “ufahamu” usiku ule ikicheza kwenye luninga katika hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa afrika…Nimewahi kuishuhudia simba mara kadhaa lakini sijawahi kuiona simba yenye mseto mzuri wa wachezaji ndani ya uwanja kama ile,kazi nzuri iliyokuwa ikifanywa na simba ile iliifanya iaminike sana kwa mashabiki wake akina Mzee Mayeka,hakika mzee wangu ni shabiki wa simba haswa..ile simba ilimuaminisha ushindi hata kabla haijakanyaga taifa kucheza na mwarabu au sheikh amri abeid kucheza na AFC au palsons ya askofu Mollel,Kambarage kucheza na Kahama united,Sokoine kucheza na Tukuyu au prisons..kote ambako simba ile ingetia mguu tayari Mzee wangu Mayeka alishaamini isingemuacha mtu salama na hili lilizidi kuiboresha desturi yake ya kutupelekesha kuchimbia ile Bendera yake yenye rangi nyeupe na nyekundu nje ya nyumba yetu kila siku asubuhi ambayo jioni yake simba ingecheza…Simba ile achilia mbali kuwatoa “kibahati” zamalek iliweza kuwaduwaza 2-1 enyimba ya Daniel Okpara,Onyekachi okonkwo na kipa wao Vincent Enyeama mbele ya Mzee Fredrick Sumaye na mamia ya wale waimba “kidedea” walioongozwa na Mzee MagomaMoto pale shamba la bibi,..Nakumbuka vizuri pia kuwa hulka ya ushindi  ilizaa imani kubwa ya mashabiki kwa timu hii yenye makao makuu pale kariakoo,hali iliyojenga ujasiri na ari kwa wachezaji..unalikumbuka lile tukio la juma kaseja kudaka ile penalti ya Numba Mumamba wa Zanaco FC(kwa sasa ndiye kocha mkuu) ya Zambia mwaka 2004? Mashabiki walikuwa wakiimba jina la Juma muda ambao penalti ile ya mwisho ilikuwa ikienda kupigwa,juma naye aliwajibu kiitikio kwa kupangua penalty ile....
Leo najaribu kutathimini nagundua kuwa simba ile ilikuwa na mseto wa wachezaji wenye vipaji haswa ,na wote walikuwa ni wazalendo wa hapahapa nchini,simba ile iliyokuwa ikiwatoa jasho waarabu na timu za afrika ya magharibiilikuwa pia na kocha kutoka nchi jirani tu hapa Kenya hayati mzee Siang’a..usajili wa Okwi juzi umefanya nianze kujiuliza ni nani aliyewasajili viungo mahiri akina Jumanne shengo Tondola na Primus kasonzo wakati ule? Ni nani aliyekuwa anawascout akina Said Sued,Victor Costa,Christopher Alex,Steven Mapunda,Emmanuel Gabriel,Athumani Machupa,Clement Kahabuka na Lubigisa Madata, Simba ile iliweza kumbembeleza Joseph Kaniki lakini pale iliposhindikana kumsajili haikupungukiwa kitu na iliendelea kufanya vizuri siku zote..nikiwa nawaza nakumbuka pia kuwa simba ile kwa wakati ule haikuwa na afisa habari..haikuwa na mtu mwenye kutengeneza tambo nyingi zisizo na mantiki mbele ya vipaza sauti vya waandishi wa habari kama ilivyo sasa..jioni ya kuamkia mechi na Enyimba ungemsikia Kassim Dewji akiongea redioni kuelezea maandalizi ya timu yake kuelekea mchezo ule..katibu mkuu huyo angemalizia kuwaalika mashabiki wa timu yake wafike kwa wingi uwanjani kuwaunga mkono na kweli akina mzee mayeka wangetabasamu baada ya mchezo wa kesho yake licha ya kuwa waliusikiliza redioni.nagundua zaidi ya kuwa kifuani mwa jezi za simba ile palikuwa na maandishi kama K.K sukari,MeTL,na Safi unga wa ngano najiaminisha kuwa Mfanyabiashara Mohamed Dewji alisimama vyema nyuma ya timu ile ambayo ilishuhudia mafanikio makubwa pengine tangu tuingie karne ya 21…………..katika harakati za kumfanyia tohara mnyama chui kunahitajika mambo makuu mawili muhimu sana..Mosi panahitajika watu jasiri wa kumlaza chali chui mwenyewe,na hawa watu hawahitaji kuwa na nguvu tu bali pia akili na mbinu nyingi sana,Pili anahitajika NGARIBA,huyu yeye anatakiwa aweze kujitoa kushika kisu na kukiamuru kifanye kazi yake basi..pale simba kwa miaka mingi tangu Mohamed Dewji asitishe ufadhili wake pametokea kipindi cha mpito kilichoshuhudia kupotea kwa ile simba iliyowafanya akina Mzee mayeka na rafiki yake Mzee Yahewa wachimbie bendera za timu yao nje ya nyumba zao….Leo simba imewaajiri akina Ezekiel Kamwaga kama maafisa habari na kuenda Congo DRC kuwachukua Linno Musombo na Kanu Mbiyavanga,haitoshi Simba hii inaenda Mali kumchukua Komambil Keitahapa unategemea Mzee Mayeka ataitoa bendera yake na kuichimbia? Hapana,Mzee huyu hana uwezo wa kujiamini kiasi hicho tena maana Simba yake kabla haijaenda kuikabili DC Motema Pembe haina uhakika wa kuondoka na pointi 4 kati ya sita za kanda ya ziwa ambazo wanazo Toto Africa na Kagera sugar licha ya kuwainayeFeliX Sunzu wa Zambia,baada ya hapo Simba inaamua kumbadili dereva mahiri aliyenyimwa ushirikiano na “wenye” gari lao Mzee Rage na kumpa usukani Evans Aveva kutoka kundi la “wenye” simba, wanachama wanamwamini kupita kiasi na kuamini kuwa huyu ndiye NGARIBA ambaye angalau ataweza kufanikisha tohara ya chui iliyowashinda wengi,Aveva anaingia na timu ya mangariba wenzake kutoka Friends of Simba ili wamsaidie kumlaza chali chui..anaajiri makocha watatu ndani ya miaka mitatu..anashirikiana na kamati yake ya usajili inayofanya kazi “ya usajili” hadi pasipo na usajili lakini wote wanaishia kuraruriwa na chui huyo huku timu haipandi ndege kwa misimu takribani minne.huku nje anambadili Kamwaga na kumpa shabiki damu Haji Manara uafisa habari,Huyu yeye anajitahidi kuwaaminisha mashabiki kile kisicho halisi na kuwaahidi ubingwa kila msimu pasipo hata kuwasiliana na makocha wake ambao ndio wanajua kuutengeneza uhakika wa ubingwa uwanjani na siyo mdomoni…..Nagundua kuwa kwa kizazi cha sasa Mo dewji ndiye ngariba pekee anayeweza kuiwezesha tohara ya chui iliyoshindikana pale Simba Sc,Dewji alikuwa ngariba mkuu kipindi kile akina Kassim dewji wakimsaidia kumlaza chali chui na hivyo aliwasaidia kumaliza kazi ile..Dewji aliweza kushirikiana vizuri na “kamati ya usajili” ya wakati huo na kuwapata wachezaji wenye uwezo tena hapa hapa nchini,naamini dewji anawakumbuka vizuri watu aliofanya nao kazi wakati ulekiasi kwamba anaweza kuwatumia hata leo maana hawa waliopo sasa hawaijui vizuri kazi yao kiasi cha kushindwa kuvumbua wachezaji na kumfanyia usajili mchezaji mmoja mara tatu ndani ya misimu 8,na haikushangaza ujio wa Dewji umeleta ubingwa wa FA kwa simba na nafasi ya pili msimu uliopita ambapo kidogo Simba imezidiwa tofauti ya magoli na bingwa, Dewji akipewa timu hahitaji sana kuwa  na wahamasishaji kama Haji manara,yeye anaamini zaidi katika kufanya uwekezaji wa moja kwa moja katika miundombinu ya soka la kileo kama kufanya usajili madhubuti na kuandaa timu imara ya vijana kwa kizazi kijacho(ameyaongelea haya kwenye mpango mkakati wake)anaweza   kukusanya watendaji makini wa kumsaidia kuifikisha juu simba,bahati nyingine MoDewji ni “Money in the bank” kiasi kwamba pale hana shida kusajili wachezaji bora na mahiri hata kwa gharama kubwa,..ni kama hivi leo tunavyosikia amewaleta Niyonzima na Okwi na bado atawalipa mshahara wao na hata wale wengine atawalipa posho msimu mzima,..leo hata wale wanaopinga mchakato wa yeye kupewa timu wanashangilia msaada anaoutoa wakati huu wa usajili na kusahau ya kuwa wanapaswa kumkabidhi rasmi kisu amalize rasmi kazi ya kumfanyia tohara huyu chui aliyewashinda…
Imeandaliwa na MWANAMAYEKA
Kwa Hisani ya #Official Toshi Newz


Comments