KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA KIFO CHA MAMA YAKE (PRINCESS DIANA), PRINCE HARRY HAJAFURAHISHWA NA HILI.

  
Prince Harry alipofanya mahojiano na mtandao wa Daily Mail juzi

Ikiwa ni takribani miaka kumi na tisa na miezi mitano tangu kufariki kwa mke wa Kwanza wa mtoto wa malikia wa Uingereza Prince Charles wa Wales, mtoto wake wa pili wa kiume Prince Charles amesema kuwa hafurahishwi na kitendo alichofanyiwa wakati wa shughuli za maombolezo na kumuaga Mama yake wakati ule.

Prince Harry (miaka 12) wa pili kutoka kulia,akiwa na kaka yake Prince Philipo (miaka 15) wakati wa maombolezo pembeni ya jeneza lenye mwili wa mama yao Princess Diana September,1997 

Prince Charles anadai kuwa haikuwa sawa kwake yeye kama mtoto wa miaka kumi na mbili kuandamana nyuma ya jeneza la mama yake  huku maelfu ya watu wakifuatilia tukio hilo  mubashara kwa njia ya televisheni wakati wa msafara wa kutembeza jeneza lenye mwili wa Princes Diana katika viunga mbilimbali vya jiji la London, Prince Charles anaamini kuwa watoto wadogo hawapaswi kuhusishwa moja kwa moja kwenye matukio kama yale,

Prince Harry (wa pili kulia), Prince Phillip (wa tatu kulia) wakati wa maandamano ya kuaga mwili wa mama yao Princess Diana mjini London September,1997 na wa kwanza kulia ni Baba yao Mwana Malkia Prince Charles 

Marehemu Princess Diana alifariki kwa ajali ya gari jijini Paris Ufaransa tarehe 31 agosti 1997

Written by MWANAMAYEKA

Designed by CHAX C

Comments