"HARUNA NIYONZIMA": INUNULIE BETRI JIPYA HIYO SAA YAKO.



        HARUNA NIYONZIMA:INUNULIE BETRI JIPYA HIYO SAA YAKO
Moja ya nguzo na kanuni sahihi  katika njia ya kufikia mafanikio ya hapa duniani ni matumizi sahihi ya MUDA, imekuwasuala la kawaida kwa vijana wengi wa kileo wakitumia saa kama mapambo tu ya kuongezea muonekano wa nyumba au labda mwili (saa za mkononi) japo kiuhalisia kazi ya saa ni kumuonyesha MUDA yule mtumiaji wake ….muda wowote kuanzia hivi sasa Haruna niyonzima anatangazwa kuwa mchezaji ghali zaidi kuwahi kukipiga kwenye ligi ya mpira wa miguu hapa Tanzania …Ndiyo ni kweli anasaini mkataba wa miaka miwili Simba SC kwa dau la takribani millioni 150 huku ikisemekana pia akipewa nyumba ya kuishi na watoto wake wakisomeshwa bure… Niyonzima amekuwa mwerevu sana… na amekuwa mwerevu hata kuliko wengi wetu ambao leo tunamtukana na kuchoma jezi yake eti kisa amehamia timu ya watani wetu wa jadi na kusababisha kejeli nyingi kutoka upande pili wa mitaa ya kariakoo….Uamuzi wa Niyonzima umekuja wakati sahihi kabisa,ni wakati sahihi kwake na kwa wanasoka na wapenzi wa soka la Tanzania ,ni wakati ambao Wachezaji na wadau wa soka tulikuwa tunajiuliza maana halisi ya neno PROFESSIONALISM kwenye soka la kileo…. Haruna anazidi kutufungua kuwa zaidi ya burudani soka ni mchezo wa kulipwa kwa dunia ya leo..na ili ukulipe ni sharti uitumie vizuri saa iliyopo mkononi mwako….ukumbuke vizuri MUDA ulionao kabla haujageuka kuwa historia, Mwanasaikolojia Abraham Muslow aliwahi kusema “mtu pekee ambaye unapaswa kupambana kumzidi ni yule uliyekuwa jana “ ..Haruna amesanuka na kuitizama zaidi saa yake,baada ya hapo akageuza shingo na kumuangalia Haruna Akizimana Niyonzima mwenyemiaka minane pale gisenyi-Rwanda,akagundua kuwa Haruna yule bado anamdai maisha mazuri zaidi aliyoishi kuyaota yatakuja kupitia miguu yake ,…Niyonzima siyo Nadir Cannavaro ambaye huenda tangu anakua  alikuwa na ndoto za kuchezea Yanga na Simba,Haruna yeye amekua na ndoto ya kutengeneza pesa kwa kuchezea Simba, Yanga na zinginezo ziitwazo klabu za soka ….Asante HARUNA NIYONZIMA ,sasa unaweza kuipa zawadi ya betri jipya hiyo saa yako ya mkononi kwa kukupa thamani sahihi kwa wakati sahihi ..THIS IS FOOTBALL

By MwanaMayeka
Written by MWANAMAYEKA
Designed by CHAX C

Comments