STAR "ALI KIBA" AWA MMILIKI NA DIRECTOR WA "ROCKSTAR4000".

Hit maker wa Aje, Alikiba baada ya kufanya kazi na kampuni ya usimamizi wa kazi zake ya Rockstar4000 kwa takriban miaka 6, Jumatatu hii ametangazwa rasmi kuwa mmoja kati ya wamiliki wa kampuni hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Rockstar4000, Muimbaji huyo amekuwa mmoja kati ya wamiliki wa kampuni hiyo, pia ni Director of Music and Talents.
“King Kiba alitangazwa rasmi kuwa sehemu ya wamiliki wa Kampuni ya Rockstar4000 Music Entertainment Co & Rockstar Television,” Ilisemwa Taarifa hiyo kwenye Media mbalimbali.
“Ali kiba kwa sasa amekuwa sehemu [Kiongozi] wa wasanii walio chini ya Rockstar4000 pia ni Director of Music And Talents,”
Rockstar Television inajishughulisha na Utengenezaji wa vipindi vya mastaa tofauti kutoka nchi mbalimbali na kuvisambaza katika vituo vya Television vya kimataifa.
Kwa sasa nchini Tanzania kampuni hiyo inamsimamia “Baraka The Prince”, 
 “Lady Jay Dee” pamoja na yeye mwenyewe[Ali Kiba].


BY CHAX C

Comments