ZARI THE BOSS LADY AMJIBU DIAMOND PLATINUMZ BAADA YA KUTOA MANENO YA HASIRA KWENYE PICHA YAKE.



Dakika chache zilizopita mwimbaji wa Bongofleva Diamond Platnumz alionekana kukasirishwa na picha ya mpenzi wake ‘Zari‘ kuonekana na Mwanaume kwenye spa katika picha zilizosambaa.

Maneno ya Diamond Platnumz baada ya hiyo picha ni haya >>> “Ndio maana wakati mwingine naonaga bora tu nile na kusepa…. maana hawathaminikagi wala kuaminika hawa"

“Baada ya maneno hayo ya Diamond, Zari nae ametuma post mbili kutolea ufafanuzi hizo picha kwa kuandika kuwa Mwanaume aliyeonekana nae ktk picha ni Binamu wa Marehemu Ivan na hiyo picha yao ilipigwa na Mke wake.

Kwenye post nyingine Zari aliweka picha nne kwenye picha moja na kuonyesha watu aliokua nao siku hiyo na kuonyesha kukasirishwa na waliozisambaza hizo picha…. akaandika And to the fools circulating this nonsense mnitole nja zak****e kwa maisha yangu punda nyinyi…..”






Tunaamini haya yatapita na amani itarejea…. bado tungependa kuwaona pamoja wakifurahia mapenzi yao


Source:Raha za Walimwengu

Designed by CHAX C

Comments