MREMBO "NISHA" ADAIWA KUMCHUKUA "BWANA WA SHILOLE".



Staa wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’.
STAA wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ anadaiwa kuwa kwenye mahaba motomoto na aliyekuwa mpenzi wa msanii mwenzake, Zuwena Mohammed ‘Shilole’
anayejulikana kwa jina la Boy Caro. Chanzo makini kililieleza Risasi Jumamosi kuwa, Nisha anapika na kupakua na mwanaume huyo bila hata aibu ambapo amehama Mbezi Makonde jijini Dar alikokuwa akiishi mwanzo na kuhamia Mikocheni kwa mwanaume huyo.


Msanii Zuwena Mohammed ‘Shilole’ alipokuwa na mpenzi wake huyo.
“Mapenzi ya Nisha na Boy Caro siyo siri tena kwani wanaishi pamoja, wanapika na kupakua hata hivi karibuni aliweka mtandaoni picha ya mkono wa mwanaume uliochorwa tatuu ambapo watu waligundua kuwa ni wa Boy Caro kwani aliichora wakati yupo na Shilole.


Source:Raha za Walimwengu

Designed by CHAX C

Comments