ANTONIO CONTE : KUNA BOSI MMOJA TU CHELSEA.



ANTONIO CONTE :KUNA BOSI MMOJA TU CHELSEA
Mabilionea wanaziamini sana BENKI kuliko hata walinzi wao binafsi (personal body guard), bilionea anaamini BENKI ndiyo inalinda uhai wake, bilionea anaamini BENKI ndiyo inampa thamani yake mbele za watu na siyo zile suti ghali za chapa adhimu ya Hugo boss,wakati weweunaamini pesa huleta MAJIVUNO bilionea anaamini pesa huleta MAVUNO kiasi kwamba yeye anamini zaidi kwamba hata akipanda miwa mbele ya pesa haishindikani kuvuna mihogo… Hii ni hulka inayotawala fikra za mabilionea wengi akiwemo Roman Abramovic….
Kuna mtu mmoja anajaribu kucheza na akili za bilionea, anajaribu kutengeneza shinikizo ili kumfanya bilionea amwamini yeye zaidi hivyo afanye analolitaka.. Mtu huyu anajaribu kujisahaulisha kuwa kitu pekee kinachoweza kumtengenezea shinikizo bilionea na kumfanya apoteze walau usingizi mmoja kwa wiki ni BENKI pekee ambako ndiko ubatizo wa jina lake ulifanyika.. Mtu huyu anaitwa Antonio Conte, nashindwa kuelewa anachokifanya na anachokiwazakwa sasa muitaliano huyu, Conte leo  anahoji  kwa nini hajapewa fungu kubwa la usajili,wakati akiwa anahoji anataharuki zaidi baada ya kugundua kuwa pesa ya usajili ipo lakini majukumu yote amepewa mkurugenzi wa ufundi Michael  Emenalo..hapa sasa Conte anachanganyikiwa, akili yake inamwambia kuwa amedharauliwa sana, akili yake inamwambia kuwa yeye ndiye BOSS wa Chelsea kwa sasa kisa ametoka kuchukua taji miezi miwili tu iliopita, akili yake inaenda mbali zaidi na kumwaminisha kuwa wakati huu alipaswa aachiwe PESA na afanye marekebisho ya kikosi kwa uhuru wake.. akili yake inaamua kusahau kabisa kuwa hicho alichokuwa anakifikiri hata Mourinho aliwahi kufikiri hivyo miezi kumi na tano iliyopita… Leo akili yake inakuja na uamuzi ambao hata yeye anauafiki haraka haraka kuwa atingishe mguu, na zaidi atingishe miguu yote miwili kwa kushirikiana na wakala wake kutengeneza tetesi kuwa eti ametengewa maslahi mazuri pale Inter Milan kama Chelsea hawatatekeleza matakwa yake kwenye usajili…… Sijawahi kuona msanii wa vichekesho kutoka Italia ila Antonio Conte amenifanya nicheke sana… anamtingishia miguu nani eti? Huyu huyu Roman Abramovic?  Ulishawahi kumuona Abramovic akitabasamu pindi Chelsea inapobeba ubingwa? Huyu jamaa hutoa matabasamu mawili kwa wakati mmoja, tabasamu la kwanza ni kama lile la John Terry la kufurahia taji la 5 la ubingwa wa EPL, tabasamu la pili ni lile la kuona msimamo na kile anachokiamini siku zote vinazidi kulipa na kuzaa matunda  vizuri pasina shaka , ni ule msimamo wake wa kubadili makocha 12 ndani ya misimu 14hukutimu ikitwaa makombe 15 tangu awe mmiliki wa Chelsea, Abramovic kama mfanyabiashara madhubuti haoni ajabu kuchukua maamuzi ambayo machoni kwa wengi yanaweza onekana magumu japo kwake ni rahisi tu kama kuvunja mkataba na kocha ndio maana anafurahi kuona kama Antonio Contealiyemletabaada ya kumfukuza Mourinho anampa ubingwa basi hata siku akimchukua Diego Simeone msimu ujao  pasina shaka atampatia ubingwa… hii ndiyo sababu anaamini yeye ndiye BOSS wa Chelsea, anaamini ujanja wake wa kubadili makocha na kununua wachezaji mahiri kwa kushirikiana na swahiba wake Michael  Emenalo ndiyo umeifikisha Chelsea hapa ilipo na siyo ujuzi wa makocha aliowahi kuwaajiri … Kwake yeye makocha huwaruhusu wachukue cheo cha umanager na hayuko radhi kuwapa uBOSS, Mourinho alijaribu kutaka kuiba uBOSS wake kilichompata anakijua… Conte anajaribu kutumia ubingwa alotwaa juzi kama ngao wakati akijaribu shabaha ya kuzipiga fikra za mmiliki wa timu anayofundisha ,Conte nakuomba utambue kuwa mrumi (Roman) abramovich hatingishiki hata kidogo na hicho unachokiona wewe ni ngao ni sawa na boksi tu maana hata muitaliano mwenzio Ancelotti alianza vizuri kukuzidi hata wewe lakini mataji yake mawili yaliishia na barua ya kuachishwa kazi tena akipewa kwenye korido za pale Goodison Park May 2011…Conte usidanganywe na hisia za mashabiki ukadhani wanakuungamkono na hizo harakati zako ambazo zimekosa umakini kuzidiwa na zile za Joram kiango wa Ben R. Mtobwa……Nimalize kwa kukupa hii lonja ya kuwa pale Chelsea maBoss walikuwepo kipindi kile wewe unacheza soka ila tangu ustaafu wanaoajiriwa ni maMeneja tu ukiwemo wewe pia…. Nikunong’oneze na hili japo usimwambie mtu ni hivi kama ulikuwa hujui “role model wa Abramovic ni Florentino Perez “
By MwanaMayeka

Written by MWANAMAYEKA
Designed by CHAX C

Comments